Mapenzi ni kama kikohozi; hayafichiki. Mapenzi haya huwasumbua watu wa rika zote. Kibaya ni kwamba mapenzi hayajui umri, jinsia, tabaka wala kabila. Mapenzi humfanya hata aliyesoma kukaa mbu mbu mbu mzungu wa reli kwa mambo yaliyo bayana na wazi kwamba hayafai wala hayatawahi tokea.
Kwa mfano, harakati za kuwatengesha wapenzi wawili waliojitosa kwenye bahari hii ya mapenzi huwa si kazi kidigo. Utafanya kazi kupita kiasi. Ni kazi ngumu.