Marende tax debate next week

Spika wa bunge Kenneth Marende amekuwa ni mwenye kumulikwa siku za hivi karibuni hasa kwa kuonekana kuwa mkaidi katika mjadala wa ushuru wa wabunge huku wachanganuzi wa kisiasa wakidai kuwa Marende hajaashiria uongozi mwema bungeni kama ilivyo katika idara nyengine za serikali.kulingana naye serikali na halmashauri ya utozaji ushuru ilihakikishia bunge kwamba marupurupu yao hayatatozwa ushuru na kusisitiza kuwa iwapo watahitajika kulipa ushuru wa ziada sheria itahitajika kubuniwa ili kutoa mwongozo dhabiti. Jee ni sheria inayobezwa au kwa wabunge kujitakia makuu?