EACC yachunguza ufisadi kwenye kaunti

News

Na Sophia Chinyezi

Takriban nusu ya kesi za ufisadi zinazochunguzwa na Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi, EACC zinahusu serikali za kaunti. Afisa Mkuu Mtendaji wa EACC, Halakhe Waqo ameieleza Kamati ya Seneti ya Sheria na Haki za Binaadamu kwamba ufisadi umekithiri katika maeneo ya mashinani na kufichua kuwa miongoni mwa kesi mia nne kumi na moja, mia mbili zinazochunguzwa kwa sasa zinahusu kaunti.

Hata hivyo EACC imejivunia kuwa na mwaka wa mafanikio ambapo imewafungulia mashtaka washukiwa kumi na wanane na kushinda rufaa miongoni mwa kesi ishirini na mbili ambazo zimekamilishwa mahakamani.

Wakati uo huo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Amos Wako amemwagiza Halakhe kuwasilisha kesi mahakamani kuzishinikiza serikali za kaunti kufuata kanuni za uongozi na maadili kwa maafisa wa serikali kabla ya uchaguzi mkuu Agosti 8 mwaka ujao.

Athletics
Kirui, Kibiwott to renew rivalry at Kip Keino Classic
Athletics
Experienced athletes set to face upcoming stars at Eldoret City Marathon
By Mose Sammy 13 hrs ago
Golf
Over 180 golfers to grace Mulembe tournament
By Ben Ahenda 18 hrs ago
Rugby
Cheetahs start training ahead of Super Series