Na Mike Nyagwoka
Watu watatu wametiwa mbaroni jijini Nairobi kufuatia maandamano yaliyofanyika kupinga hafla ya Jamhuri mapema leo chini ya kauli mbiu #TakeBackKenya. Maandamano hayo yalikuwa yakiongozwa na kundi la wanaharakati akiwamo Boniface Mwangi kabla ya maafisa wa polisi kuingilia kati na kuwatawanya kutumia vitoza machozi.
Hayo yanajiri huku hatua hiyo ya polisi ikiendelea kushtumiwa. Katika mitandao ya kijamii, Wakenya wameitaja hatua ya kuyatibua maandamano kutumia vitoza machozi kuwa ya kikoloni na ambayo inakwenda kinyume na matarajio wakati kama huu Kenya inaposherehekea miaka 53 ya kujitawala.