Premium

Mtu mmoja ameripotiwa kuaga dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya kwenye ajali ya barabarani, iliyohusisha magari 4 katika Nairobi Expressway, usiku wa kuamkia leo.

Mtu mmoja ameaga dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya kwenye ajali ya barabarani, iliyohusisha magari 4 katika  Nairobi Expressway, usiku wa kuamkia Jumapili.

Kwenye ajali hiyo ya kwanza kabisa katika Nairobi Expressway, dereva mmoja alikuwa akiendesha gari lake kwa mwendo wa kasi zaidi, hadi akashindwa kudhibiti usukani na kugonga magari mengine matatu yaliyokuwa yakisubiri kupewa idhini ya kuondoka kwenye Barabara ya Nairobi Expressway, baada ya kulipa ada za kutumia barabara hiyo.

Kamanda wa Polisi wa eneo la Athi River, Agnes Makau, amethibitishwa kwamba dereva mmoja alifariki dunia papo hapo.

Aidha, Mamlaka ya Kitaifa ya Barabara Kuu Nchini  KENHA, imesema watu waliojeruhiwa wanaendelea kutibiwa hospitalini, huku kituo cha Nairobi Expressway ambacho kiliharibika baada ya kugongwa na gari hilo kikifungwa kwa muda.

KENHA imewataka madereva kuzingatia sheria za trafiki na ishara za barabarani hasa kwenye Nairobi Expressway ili kuzuia ajali.

Kufuatia ajali hiyo serikali sasa imesema inapanga kuweka mikakati ya kukabili ajali katika Barabara ya Nairobi express Way kufuatia ajali iliyosababisha kifo cha mtu mmoja katika eneo la Mlolongo usikuwa kuamkia leo.

Msemaji wa Serikali Cyrus Oguna amesema kuna mipango ya kuweka sheria ambapo magari yatakayotumia barabara hiyo hayataruhisiwa kwenda mwendo wa kasi zaidi ya kilomita themanini kwa saa.

Oguna amewashauri waendesha magari kuzingatia sheria.

By AFP 2 hrs ago
Football
Arsenal, Liverpool fight to keep Premier League race alive
Athletics
World hammer silver medallist Kassanavoid eyes glory at Nyayo on Saturday
Athletics
Eldoret City Marathon to have a bigger 10km fun run
Athletics
'School boy' Tebogo promises to teach his seniors a lesson at Kip Keino Classic