Jaji Mkuu Martha Koome ameitaka Tume ya Uchaguzi IEBC kushughulikia kwa haraka masuala makuu yaliyosababisha kubatilishwa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017.
Akizungumza wakati wa kikao na Chama wa Wahariri Nchi kuhusu utayarifu wa Idara ya Mahakama kushughulikia kesi za baada ya uchaguzi, Koome amesema kuwa nyingi ya masuala hayo yalihusu utendakazi wa IEBC.
Koome amesema tume hiyo inastahili kuwaeleza Wakenya namna imeweka mikakati ya kuzuia kurudiwa kwa hali iliyoshuhudiwa hasa kuhusu kusambazwa na kutangazwa kwa matokeo ya kura za urais.
Kikao hicho pia kulijadili suala la wawaniaji wenye kesi mbalimbali mahakamani hasa baada ya IEBC kusema kuwa hawawezi kuzuiwa hadi rufaa walizowasilishwa zitakaposilikizwa na kuamuliwa. Jaji Daniel Musinga anaeleza amesisitiza umuhimu wa hilo kuzingatiwa.
Koome amesema jumla ya kesi 168 za kura ya mchujo zinasikilizwa na Mahakama ya Kutatua Migogoro ya Vyama Kisiasa, 29 zikishughulikiwa na Mahakama Kuu na moja katika Mahakama ya Juu.