''Fuateni ratiba.'' IEBC yaviambia vyama vya siasa

Na Carren Omae
Tume ya Uchaguzi, IEBC imesisitiza kwamba ratiba yake ya maandalizi ya uteuzi wa vyama ndiyo itakayozingatiwa. Katika taarifa, tume hiyo imesema shughuli hiyo inafaa kuanza tarehe 13 na kukamilika tarehe 26 mwezi huu. Tangazo hili linaashiria kwamba huenda chama cha ODM ambacho kilinuia kuanza uteuzi wake mapema, hakitakuwa na budi kuahirisha shughuli hiyo.

IEBC imesema ingali katika shughuli ya kuchapisha majina ya watakaowania tiketi ya vyama vya kisiasa katika gazeti rasmi la serikali.

Kwa mujibu wa sheria za uchaguzi tume hiyo inafaa kuchapisha majina hayo kabla ya siku saba kukamilika baada ya kuyapokea. Ikumbukwe makataa ya kuwasilisha majina hayo yalikamilika tarehe 5 mwezi huu.
Tangazo hili la IEBC linafuatia licha ya kufanya mkutano wa kujadili miongoni mwa masuala mengine uteuzi wa vyama na viongozi wa ODM jana. Siku chache zilizopita Kiongozi wa ODM Raila Odinga alisisitiza kwamba wataendelea na mipango yao ya uteuzi wa mapema

Related Topics

IEBC