Maafisa wakuu wa vitengo vyote vya usalama katika Kaunti ya Kilifi wamehamishwa.
Waziri wa Usalama na Masuala ya Ndani ya Nchi, Profesa Kithure Kindiki amesema iwapo ni kweli kwamba wapo maafisa waliopokea taarifa kuhusu mauaji ya Shakahola na kukosa kuchukua hatua basi hawastahili kuwa miongoni mwa wanaoendeleza uchunguzi.