Majibizano makali yameendelea baina ya pande za Naibu wa Rais William Ruto na Raila Odinga kuhusu madai ya Ruto na wandani wake kumkosea heshima Rais Uhuru Kenyatta.
Kauli ya Ruto kwamba atabuni kitengo cha mahakama cha kuchunguza miradi iliyofanywa na Kenyatta na kumwajibisha imeendelea kuibua mjadala mkali kutoka kwa wapinzani wake wanaodai kwamba yeye ni mnafiki.