Mgombea urais wa UDA, Naibu wa Rais William Ruto ameendeleza shutma dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta kwa kuisuta manifesto yake huku akimhusisha na mapungufu serikalini. Akiwahutubia wakazi wa Meru, Ruto amesisitiza kutengwa serikalini na kamwe Rais hafai kumlaumu. Aidha, amemtaka kujiondoa katika siasa za mwaka huu, akisema hashindani naye bali Raila Odinga.
Mbunge wa Kikuyu Kimani Ichung'wa kwa upande wake amemtaka Rais kuubeba msalaba wake bila kumlaumu Ruto.