Abiria wote waliokuwa katika ndege iliyohusika katika ajali Jumanne usiku kwenye Msitu wa Aberdare walifariki dunia. Mwenyekiti wa kampuni ya ndege ya Fly SAX iliyohusika ajali hiyo Charles Wako amethibitisha taarifa hizo huku akituma rambirambi kwa familia za walioaga.
Tangazo hilo limetolewa muda mfupi uliopita wakati shughuli ya kuwatafuta manusura ikiendelea.
Mapema leo Katibu wa Wizara ya Uchukuzi, Paul Maringa alisema mabaki ya ndege hiyo yalipatikana Kusini Magharabi ya msitu huo eneo la Njambini, Kaunti ya Nyandarua.