Watu watano wameuliwa kwa kukatwa vichwa na washukiwa wa kundi gaidi la Al-Shabaab kwenye Kijiji cha Salama, kata ya Mkunumbi, katika Kaunti ya Lamu.
Miongoni mwa watu waliouliwa ni mwanafunzi wa kidato cha tatu ambaye alikuwa ameenda nyumbani kwa ajili ya likizo ya katikati ya muhula.