Mshukiwa Jackson Vuti Muthangya akiwa mahakamani baada ya kudaiwa kuiba bunduki na rununu ya afisa wa polisi. Amezuiliwa kwa siku 15 hadi polisi wakamilishe uchunguzi wao dhidi yake. Picha: Kelvin Karan.
Afisa wa polisi ambaye alipoteza bunduki yake anadaiwa kuibiwa bunduki hiyo na kahaba, kisha kumsingizia mhudumu wa bodaboda. Afisa huyo ambaye hakutajwa kwenye nakala za kuomba mahakama kumzuilia mhudumu huyo wa bodaboda anaaminika kuchukua kahaba ambaye alimwibia bunduki pamoja na simu yake ya mkono, kisha kudai kuwa mhudumu huyo alijua kahaba huyo. Maafisa wa polisi walitaka Mahakama kupitia Hakimu Mkuu Edna Nyaloti kumzuilia Jackson Vuti Muthanya kwa siku ishirini ili kukamilisha uchunguzi wa wizi huo dhidi yake.