Pilipili ni matunda ya mpilipili, ni matunda ambayo sio matamu kama matunda mengine lakini ni mazuri kwa afya ya mwanadamu. Ni matunda yanayochukiwa na wengi kiasi kwamba huwezi kununua na kupelekea mtu kama zawadi, pengine akikutuma umletee. Pilipili ziko za aina nyingi na inasemekana zilitoka bara la Asia na kusambazwa hadi Marekani kabla ya kuletwa Afrika na nchi zingine ulimwenguni.
Pilipili zaweza patikana kwa rangi tofauti tofauti kama vile nyekundu, zambarau, manjano na kijani kulingana na mazingira au aina ya mmea wa pilipili. Kisayansi pilipili waeza kuziita Capsicum, kiambata ambacho hufanya pilipili kuwa na ladha kali ya uchachu na pia kuongeza ladha nzuri kwa chakula ni Capsaicin. Kuna pilipili ambazo ni kali na zingine ambazo sio kali.