Naibu wa Rais William Ruto amemsuta Gavana wa Nyamira John Nyagarama kwa kukosa kuhudhuria Harambee ya Kanisa la Kiadventista la Tente mjini Nyamira siku ya Jumamosi.
Ruto ambaye alikuwa mgeni wa Heshima kwenye hafla ya kununua Basi la Kanisa hilo alisema lilikuwa jambo la kushangaza kwa Nyagarama kukosa kuhudhuria ilhali yeye ni mshiriki wa kanisa hilo ambalo liko umbali wa mita 50 kutoka kwa makazi yake rasmi.