Kwa mujibu wa chama cha wasafirishaji mashehena kwa njia ya barabara, wanaharakati wa haki za kibanadamu na viongozi wengine Mombasa, suala tata linalohusu usafirishaji wa mizigo kupitia reli ya SGR limeishia kufanyiwa mzaha na serikali kuu.
Huku wakikariri sababu yao ya kuendeleza msururu wa maandamano mapema wiki hii, chama hicho cha wasafirishaji (KTA), kilifichua kuwa hadi kufikia mwishoni wa wikiendi iliopita amri ya kusimamisha kwa muda uamuzi huo ilikuwa bado haijatekelezwa bandarini Mombasa.