Tishio Kubwa kwa Naibu Rais William Samoei Ruto na “Team Tangatanga” sio kiongozi wa upinzani Raila Odinga bali ni Fred Matiang’i. Waziri huyo kiranja na Usalama wa Ndani ana wakosesha raha wanaRuto na nahodha wao wakihisi Matiang’i ni ? mbo ya UhuRaila 2022 kumzima mpendwa Kigogo chao Cha Mkoa wa Bonde la Ufa penyenye za kuwa Rais wa tano jamhuri hii chini ya makubaliano-siri 2013 baina URP ya Ruto na TNA ya Uhuru hatimaye kuundwa Jubilee Alliance ya sasa.
Bila shaka suluhu ya siri kati ya Uhuru na Raila mnamo Mei 9 mwaka Jana kufuatia vurugumechi za Uchaguzi mkuu 2017 umemweka Ruto na kigaro chake mataani. Kuja kwa Raila na waitifaki serikalini kumejenga ODM ya Baba Tinga na kummbomowa Ruto na wana-URP wa zamani na wengineo chini ya bendera ya Ruto nchini.