Mdahalo umezuka tangu kuteketezwa kwa mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Safaricom, Robert “Bob” Collymore na wakenya wengine mashuhuri hivi karibuni kuwa sababu yake halisi ya kupitia mfumo huo ni nini haswa.
Wakenya hao mashuhuri ambao miili yao ilipitia mfumo huo ni pamoja na aliyekuwa mwanaharakati wa uhifadhi wa Mazingira Bi. Wangari Maathai aliyefariki mwaka 2011, aliyekuwa kiongozi wa upinzani Keneth Matiba, aliiyekuwa mchezaji golf maarufu Peter Njiru, aliyekuwa waziri Peter Okondo, Askofu wa Kanisa la Kianglikana Manasses Kuria na mkewe Nyambura Kuria.