×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands of Readers
★★★★ - on Play Store
Download Now

Kizazi cha Mswahili huenda kilitokana na Mngozi na Mwarabu?

Wengi wenu mkisikia neno uswahilini unajawa na mawazo kwamba, haya ni maeneo ya watu wa hali duni, sehemu zile zinazoitwa Majengo au mitaa ya mabanda. Ni lazima kutakuwa na maisha ya kihuni huni au ukora tena kuna udaku usabasi na  uongo. Baadhi huchukua uswahilini ni kwa watu wavivu wanaopenda starehe, watu wakujipenda wataaradhi na kadhalika. Lakini kwa maana kubwa zaidi ya hiyo, uswahilini ni uafrikani, yaani kule wanakoishi waafrika tena wa hali ya kadiri au kwa lugha nzuri watu wenye kipato cha kati wastaarabu na wenye maadili, na miendo yao ya kimaisha. Licha ya hayo, maeneo mengi ya aina hiyo huwa yana msongamano wa watu.

Kwa sababu maisha katika maeneo hayo huwa nafuu kiasi. Kutokana na hali hiyo, wenye pesa wakakuita uswahilini, maana mchanganyiko huo wa makabila tofauti tofauti, dini na desturi  unalazimisha wakazi hao kuzungumza kiswahili ndio  lugha kuu ya mawasiliano yao, kikifatiwa kidogo na kingereza, kisha makabila yao pale wanapo kuwa wamekutana watu wa kabila moja na wapo mahala fulani pamoja, wanajikuta wanazungumza lugha yao.

Get Full Access for Ksh299/Week
Uncover the stories others won’t tell. Subscribe now for exclusive access
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in