Wakati jamii ya Waluo walipohamia nchini Kenya kutoka maeneo ya Uganda na Sudan, walijitafutia makao yao karibu ziwa la Victoria mnamo karne ya 15 wakiongozwa na Mzee mmoja kwa jina la Ramogi Ajwang ambaye alichukuliwa kama miongoni mwa mashujaa wa mwanzo.
Vizaliwa waliozaliwa hatimaye walikuwa na hamu ya kufi kia kiwango chake cha umaarufu. Barubaru walimuenzi na kutamani kuwa mfano wake. Kulingana na wana historia, wanasema hiki ndicho chanzo cha mahiri wa siasa ya Nyanza, akiwemo Oginga Odinga kuwa sababu yakujibatiza jina la “Ja-Ramogi” ikimaanisha “Ni ukoo wa...” (Jaramogi Oginga Odinga) na kweli Mzee aliambulia kuwa wa ajabu, kuogopesha, kuheshimika na kinga ya jamii nzima ya Nyanza.