Kifo cha ghafula cha aliyekuwa Rais alochaguliwa kihali kule Misri Mohammed Morsi juma lilopita katika mahakama kimewashtua wengi na kuacha maswali mengi.
‘Kwa niaba ya watu wa Uturuki tunatowa risala za rambi rambi kwa familia ya Morsi kwa kifo chake’ asema Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na kumlaumu mtawala wa sasa wa Misri Abdel Fattah El-Sisi kwa masaibu na kifo cha Morsi.