Jopo la Boko Haram kusababisha maafa nchini Nigeria kaskazini kila kukicha ni jambo la kusikitisha sana. Kufaulu kwa Rais Muhammadu Buhari kwenye uchaguzi Nigeria kunatoa matarajio mapya ya kupata suluhu kwa jambo hili lililokumba nchi nzima ya Nigeria.
Linaloshangaza ni kwamba kikundi kidogo cha magaidi kama Boko Haram linaweza kusababisha maafa vile wamefanya eneo za Borno na Maiduguri. Ukinoa bongo, inaonekana bayana kwamba kunao maafisa kwenye idara za kiusalama Nigeria wanaounga mkono wanamgambo wa Boko Haram.