Mahojiano na Maina Njenga

Sote tunamfahamu Maina Njenga na uhusiano wake na kundi haramu la Mungiki, kundi ambalo kwa sasa amekana kuhusika nalo.  Maina anakabiliwa na kesi mahakamani kufuatia kuzuka kwa vurugu kwenye kanisa lake mtaani Garden wiki iliyopita.  Frank Otieno alifanya naye  mahojiano ya moja kwa moja  ili kubaini chimbuko la misukosuko yake  mbali na  madai anayoyatoa  kwamba wapo watu wanaotaka kumuangamiza.