Sofapaka on CAF Cup return leg-Swahili

Baada ya kulazwa kwa 3-0 na timu ya Club Africain kutoka Tunisia nchini humo kwenye mechi ya mchujo ya raundi tatu ya dimba la klabu bingwa bara Afrika timu ya SOFAPAKA chini ya ukufunzi wa kocha Francis Kimanzi iko mbioni kurekebisha makosa waliofanya nchini Tunisia huku wakitegemea pakubwa mashabiki wao itimiapo wikendi hii watakapochuana na Club Africain kwenye mechi ya marudiano katika uga wa Nyayo.