Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa amewakosoa vikali maafisa wa polisi kwenye Kaunti ya Kilifi kwa madai kuwa wanachangia kusambaa kwa virusi vya korona.
Kulingana na Jumwa, maafisa hao wamekuwa wakiwalazimisha wakazi kujifunga kitambaa cha aina yoyote puani na mdomoni wakitishia kuwakamata na kuwafungulia mashtaka.