Miaka nenda miaka rudi, kivuko cha Likoni Ferry kimekuwa kikifanyiziwa tambiko maalum na Wazee wa Kidigo ambao wamekuwa na jadi zao za kimila kwamba pepo wa bahari lazima kufanyiwa karamu yao kwa kuchinjwa ng’ombe mwakani na kutupwa ndani ya bahari hindi.
Kulingana na wazee hawa, tambiko la kumwaga damu baharini hususani katika kivuko cha Likoni ni kuepuka majanga ya maafa ama ajali za kufa maji ambazo wahenga huamini kuwa endapo matambiko ya aina hiyo hazitekelezwi kwa wakati ufaao, pepo hao wa baharini huja kama nuksi kusababisha ajali ya aidha gari kuzama na watu baharini au mtu kujirusha majini bila simule.