Maafisa zaidi wa Dci wafanyiwa uhamisho.

Zaidi ya maafisa mia moja wa polisi wanaohudumu katika afisi za Idara ya Upepelezi, DCI kote nchini wamefanyiwa uhamisho.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Upelelezi DCI, George Kinoti amesema maafisa mia moja ishirini na sita watatakiwa kuripoti kwenye vituo vyao vipya  kufikia tarehe mosi mwezi ujao.

Watakaoathiriwa ni pamoja na mainspekta wakuu watatu, mainspekta sita, senior sergent na sergent kumi na saba, corporal thelathini na watano na constable sitini na watano.

Kinoti amesema mabadiliko hayo yanalenga kuimarisha utendakazi wa maafisa hao. Aidha amesema maafisa waliohudumu kwa muda katika vituo hivyo watahamishwa.

Kuhusu mafunzo ya maafisa hao, Kinoti amesema zaidi ya maafisa mia tano wanafanyiwa mafunzo kote nchini lengo likiwa ni kuboresha utendakazi wao.

Related Topics

dci