Rais Uhuru Kenyatta ameongoza hafla ya kukifungua tena kiwanda cha nguo cha Rivatex kilichoko mjini Eldoret. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais amesema kwamba serikali itaendelea kuwekeza zaidi ili kuimarisha sekta ya viwanda nchini. Amesema kando na hayo, ufunguzi wa leo utakuwa wa manufaa makubwa kwani vijana wengi watapata kazi huku wakulima wa pamba pia wakinufaika, kwani watapata soko kwa zao lao.
Kuhusu kilimo cha pamba iliyobadilishwa kijenetiki yaani GMO rais ameziagiza idara zinazohusika na kilimo, afya, na elimu kuharakisha mpango wa kuanza kilimo cha pamba hiyo, inayojulikana kuwa BT Cotton.