Nyoka yawashambulia wakazi wa Koredo Homa Bay.

Wakazi wa Koredo kwenye Kaunti ya Homa Bay, wanaishi kwa hofu kufuatia ongezeko la visa vya nyoka kuwashambulia.

Malalamiko yao yanajiri siku chache tu baada ya mwanamume mwenye umri wa makamo kushambuliwa na nyoka aina ya python akiwa shambani kabla ya wananchi kumwangamiza nyoka huyo.

Wakazi wanasema nyoka hao wamekuwa wakirandaranda ovyo kutoka kwenye misitu ya Rawi, Kobiero, Lwasi, na Oyaore wakisababisha hofu miongoni mwao. Akithibitisha kauli za wakazi Naibu Chifu wa Koredo David Opera amesema nyoka hao wamekuwa tisho hasa kwa mifugo.

Opera  sasa ametoa wito kwa Shirika la Huduma za Wanyamapori, KWS kuingilia kati suala hilo ,akisema wakazi wanaendelea kuishi kwa hofu.

Related Topics

Homa Bay Snakes