Mwanahabari Mkongwe wa Radio Citizen, Mohammed Juma Njuguna ameaga dunia. Njuguna amefariki mapema leo katika Nairobi Hospital alipokuwa akipokea matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Inaarifiwa Njuguna amekuwa akiugua maradhi ya kisukari na shinikizo la damu. Sauti ya Njuguna inatambulika sana katika utangazaji wa soka kwa miaka mingi akitumia kauli “Kadenge na mpira” .