Uchaguzi wa viongozi wa Chama cha FORD Kenya katika maeneo bunge yote kwenye Kaunti ya Trans Nzoia unaendelea.
Kwenye Eneo Bunge la Saboti uchaguzi huo umekamilika muda mfupi uliopita huku baadhi waliokuwa wakiwania nyadhifa mbalimbali akiwamo Elisha Khalai aliyewania nafasi ya mwenyekiti, akielezea kutorishwa na uchaguzi huo na kwamba majina ya baadhi ya wawaniaji yaliondolewa kwenye orodha ya wapigakura.
Hata hivyo msimamizi wa uchaguzi huo, kasisi John Okumu amesisitiza kwamba uchaguzi huo umekuwa huru na haki.