Viongozi wa Somalia wazuiwa kuingia nchini

Mzozo wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia huenda ukaibuka tena baada raia watatu waliokuwa na pasipoti za kidiplomasia kunyimwa kuingia nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, JKIA jana jioni.

Kupitia mtandao wa Twitter Kituo cha Radio cha Dalsan FM nchini Somalia imewatambua watatu hao kuwa Osman Libah ambaye ni Naibu Waziri wa Maji na Kawi na maseneta Ali Hassan na Zamzam Dahir.

Waziri Liban alikuwa amezuru humu nchini kuhudhuria uzinduzi wa Kongamano la Uwekezaji la EU Trust Fund mapema leo.

Inaarifiwa juhudi za Ubalozi wa Somalia humu nchini kuingilia kati ziliambulia patupu huku Waziri wa Masuala ya Kigeni, Monicah Jumah akikosa kupokea simu.

Related Topics

Somalia Kenya