Viongozi wa Kaunti ya Marsabit wametoa wito kwa serikali kuimarisha usalama kwenye eneo la Forole kufuatia kisa ambapo wafugaji 11 waliuliwa siku ya Jumatatu.
Inaaminika mauaji yao yalitekelezwa na maafisa wa polisi kutoka taifa jirani la Uganda waliovuka mpaka na kuingia nchini. Inaarifiwa wakati wa kisa hicho, polisi wa akiba kwenye eneo hilo walikuwa wamepokonywa silaha zao. Hii hapa kauli ya mmoja wa viongozi hao.