Mauaji yakithiri Kakakega huku bawabu mwingine akiuliwa

Katika misururu ya visa vya mauaji kwenye Kaunti ya Kakamega, bawabu mwingine ameuliwa katika eneo la Maraba usiku wa kuamkia leo huku polisi wakisema kwamba huenda ni kisa cha uhalifu wa kawaida.

Kwa upande wake, Seneta wa Kakamega Cleopas Malala ameitaka idara ya polisi kuimarisha usalama huku akitowa wito kwa vituo vya polisi kwenye kaunti hiyo kupewa vifaa vitakavyowasaidia kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

OCPD wa Kakamega John Matsili amekiri kuwepo kwa ukosefu wa vifaa kama vile magari ya kutosha kuendesha shughuli zao huku akitoa wito kwa raia kushirikiana na maafisa wa usalama kudumisha amani.

Wito huu unajiri wakati jumla ya watu kumi na wawili wakiripotiwa kufariki dunia eneo bunge la Matungu, Kaunti io hiyo katika kipindi cha wiki tatu zilizopita pekee.