Ujumbe wake wa twitter ulijiri baada ya kauli ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini, CA, Francis Wangusi kwamba laini za watakaokosa kujisajili baada ya muda uliowekwa kukamilika zitazimwa, hivyo kutopata huduma kama vile kutuma na kupokea pesa za M-pesa, Airtel Money na hata kutoa pesa katika benki wakitumia kadi za ATM.
Akizungumza mjini Kisumu Wangusi amesema baada ya muda huo kukamilika, watawasiliana na kampuni za mawasiliano kuwasaidia katika kuzifunga laini za wale ambao watakiuka agizo la serikali kuwataka kujisajili.
Amesisitiza kwamba mpango wa Huduma Namba unalenga kurahisisha huduma za serikali katika kuwakabili walaghai.
Mpango wa Huduma Namba ulizinduliwa wiki mbili zilizopita na unaendelea kwenye maeneo yote nchini. Jumla ya watu milioni nane wamesajiliwa kufikia sasa.