Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

Serikali kuzima laini za simu za wale ambao hawatajisajili kwa Huduma Namba

Vitengo viwili vya serikali leo hii vimetoa maelezo ya kukanganya kuhusu usajili wa Huduma Namba. Muda mfupi baada ya Mamlaka ya Mawasiliano, CA kutoa taarifa kwamba laini zote za simu za wale ambao hawatakuwa wamejisajiliwa kupata Huduma Namba zitafungwa kufikia tarehe 15 Mei, kitengo kingine cha serikali kimejitokeza na kauli tofauti. Msimamizi wa Kitengo cha Kufanikisha Miradi ya Serikali ya Jubilee katika ofisi ya Rais, Presidential Delivery Unit, Nzioka Waita amesema kuwa hakuna Mkenya atakayelazimishwa kujisali kwa Huduma Namba. Katika ujumbe wake wa twitter, Nzioka amesema hitaji hili linaendana na agizo la mahakama kwamba yeyote asilazimishwe kusajiliwa kupata Huduma Namba.

Ujumbe wake wa twitter ulijiri baada ya kauli ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini, CA, Francis Wangusi kwamba laini za watakaokosa kujisajili baada ya muda uliowekwa kukamilika zitazimwa, hivyo kutopata huduma kama vile kutuma na kupokea pesa za M-pesa, Airtel Money na hata kutoa pesa katika benki wakitumia kadi za ATM.

Akizungumza mjini Kisumu Wangusi amesema baada ya muda huo kukamilika, watawasiliana na kampuni za mawasiliano kuwasaidia katika kuzifunga laini za wale ambao watakiuka agizo la serikali kuwataka kujisajili.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Related Topics

Huduma Namba Simu