The Standard Group Plc is a
multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper
print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key
influence in matters of national and international interest.
Vitengo viwili vya serikali leo hii vimetoa maelezo ya kukanganya kuhusu usajili wa Huduma Namba. Muda mfupi baada ya Mamlaka ya Mawasiliano, CA kutoa taarifa kwamba laini zote za simu za wale ambao hawatakuwa wamejisajiliwa kupata Huduma Namba zitafungwa kufikia tarehe 15 Mei, kitengo kingine cha serikali kimejitokeza na kauli tofauti. Msimamizi wa Kitengo cha Kufanikisha Miradi ya Serikali ya Jubilee katika ofisi ya Rais, Presidential Delivery Unit, Nzioka Waita amesema kuwa hakuna Mkenya atakayelazimishwa kujisali kwa Huduma Namba. Katika ujumbe wake wa twitter, Nzioka amesema hitaji hili linaendana na agizo la mahakama kwamba yeyote asilazimishwe kusajiliwa kupata Huduma Namba.
Ujumbe wake wa twitter ulijiri baada ya kauli ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini, CA, Francis Wangusi kwamba laini za watakaokosa kujisajili baada ya muda uliowekwa kukamilika zitazimwa, hivyo kutopata huduma kama vile kutuma na kupokea pesa za M-pesa, Airtel Money na hata kutoa pesa katika benki wakitumia kadi za ATM.
Akizungumza mjini Kisumu Wangusi amesema baada ya muda huo kukamilika, watawasiliana na kampuni za mawasiliano kuwasaidia katika kuzifunga laini za wale ambao watakiuka agizo la serikali kuwataka kujisajili.
Premium Article
Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.
Journalism can't be free because the truth demands investment.
At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate,
factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the
pursuit of credible journalism.