Serikali ya Marekani imempokonya viza Mkuu wa Mashtaka wa Mahakama ya ICC, Fatou Bensouda kufuatia hatua yake ya kuchunguza mauaji kati ya Marekani na Afghanistan.
Katibu Mkuu wa Marekani, Mike Pompeo amesema Marekani iliamua kuwapokonya viza maafisa wote wa ICC kufuatia madai kwamba wanachunguza visa vya mauaji dhidi yake.