Mvua kubwa kunyesha Garissa na kaunti nyingine leo hii.

Idara ya Utabiri wa Hali ya Anga imeonya kuwa mvua kubwa inatarajiwa kunyesha kwenye kaunti za Wajir, Garissa, Mandera, Isiolo na Marsabit kuanzia leo hadi Alhamisi.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Idara hiyo aidha imesema kuwa mvua hiyo itakuwa zaidi ya milimita 30 na huenda ikanyesha kwa saa 24 mfululizo.

Tahadhari hii inajiri wakati wananchi maeneo mbalimbali hususan Kaskazini mwa Nchi wakiendelea kulalamikia ongezeko la viwango vya joto hususan nyakati za usiku.