Afisa wa Flying Squad auliwa Taita Taveta.

Afisa wa kitengo cha Flying Squad ameuliwa usiku wa kuamkia leo na washukiwa wa uhalifu mjini Taveta kwenye Kaunti ya Taita Taveta.

Afisa huyo alikuwa na wenzake wakati alipopigwa risasi na watu wawili ambao vilevile wamehusishwa na uhalifu uliotekelezwa mjini Mombasa na kunaswa katika kamera za CCTV.

OCPD wa Taveta, Lawrence Maroa anasema kuwa marehemu aliripotiwa kuaga dunia katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Taveta.

Aidha, Maroa amedokeza kwamba marehemu alikuwa akiwaandama washukiwa hao kutoka Mombasa na kwamba alikuwa akishirikiana na wenzao mjini Taveta. Washukiwa hao walifanikiwa kutoweka kwa pikipiki kuelekea taifa jirani la Tanzania.

Related Topics

flying squad