Mfanyabiashara mmoja maarufu jijini Mombasa amefikishwa mahakamani baada ya kunaswa wikendi akiwa na kilo moja ya dawa aina ya heroin zenye thamani ya shilingi milioni 1.5.
Abdul Majid Msallam Timami wa umri wa miaka 47 amefikishwa katika Mahakama ya Mombasa ambapo anasomewa mashtaka dhidi yake.