Ichungwa awataja baadhi ya Wabunge wa ODM kuwa fisadi

Huku vita dhidi ya ufisadi vikiendelea nchini ,mbunge wa Kikuyu Kimani Ichungwa amewalahumu baadhi ya Wabunge wa chama cha ODM ambao amedai ni fisadi huku wakiendelea kuwashtumu wengine. Amesema ni wazi kuwa baadhi ya mahasimu wa Naibu Rais William Ruto wamehusika katika sakata mbalimbali.

Akizungumza katika kanisa la PCEA Jijini Nairobi, mbunge huyo amesema iwapo Serikali inataka kuhakikisha amani katika taifa nzima ,ni lazima kila kiongozi aheshimu kazi yake.

Aidha amemtaka Rais Uhuru kenyatta na Naibu wake William Ruto, kuangazia ajenda nne kuu za serikali.

Hafla ya hiyo imehudhuriwa na Naibu wa Rais William Ruto na viongozi wengine wa kisiasa.

Related Topics