Mudavadi alalamikia ufisadi unaohusishwa na miradi mbalimbali ya serikali

Kinara wa Chama cha ANC, Musalia Mudavadi amechukua fursa ya kongamano la wataalam wa idara mbalimbali linalojulikana kama Future of Kenya Professionals ambalo limekamilika leo Jijini Mombasa, kuendelea kuonesha kukerwa kwake na suala la ufisadi ambao umeandama ujenzi wa miradi ya mabwawa ya Arror na Kimwarer kwenye Kaunti ya Elgeyo - Marakwet.

Mudavadi amesema ni jambo la kusitikisha kuona kwamba fedha zilitengewa miradi hiyo ilhali haijatekelezwa kufikia sasa. Ameeleza kugadhabishwa na jinsi ambavyo baadhi ya walioathiriwa na ujenzi wa miradi hiyo hadi sasa hawajalipwa fidia.

Kadhalika amewalaumu baadhi ya wataalam kwa kukubali kuhusishwa kwenye visa vya ufujaji wa fedha za umma hasa zilizotengewa utekelezwaji wa miradi mbalimbali.

 

Related Topics

Kimwarer