Waziri wa Masuala ya Ndani ya Taifa Daktari Fred Matiang'i, amesema serikali kamwe haita wavumilia maafisa wazembe kuhudumu katika vitengo mbalimbali huku wananchi wakitaabika kutokana na utendakazi duni.
Kwenye kikao na wakazi wa Lamu mapema leo, waziri Matiang'i amesema ni wajibu wa viongozi wa Serikali kutelezaji majukumu yao kwa mujibu wa sheria huku akisisitiza umuhimu wa ushiriano baina ya maafisa wa serikali.