Gavana wa Kaunti ya Turkana, Josephat Nanok amefanya mabadiliko katika Baraza lake la Mawaziri huku mawaziri wanne wakiathirika. Jennifer Nawoi ambaye alikuwa Waziri wa Utalii, Utamaduni na Mali Asili amehamishwa katika Wizara ya Biashara , Jinsia na Vijana huku nafasi yake ikichukuliwa na Charles Ewoi Lokiyoto ambaye awali alikuwa katika Wizara ya Usiamamizi wa Umma na Masuala ya Dharura.
Esther Lokiyo Lokwee vileviel ameondolewa katika Wizara ya Ardhi na Miundo Msingi hadi wizara hiyo ya usimamizi wa umma na masuala ya dharura.