Mhubiri wa Kanisa la Neno Evangelism, James Ng'ang'a ameshtakiwa kwa kumtishia maisha mwanahabari wa runinga ya Citizen, Linus Kaikai na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki mbili.
Ng'ang' amefikishwa katika Mahakama ya Kiambu baada ya kuzuiliwa katika Makao Makuu ya Idara ya Upelelezi - DCI, baada ya kukamatwa Jumapili wiki iliyopiya kwa kumtishia maisha Kaikai pamoja na kuchochea ghasia.