Huku familia za watu 157 walioaga dunia wakisubiri kufunga ukurasa wa maombolezo kwa njia mbalimbali hofu waliyokuwa nayo wengi kuhusu kilichosababisha ajali hiyo ya ndege kimethibitishwa kufuatia vidokezo vya awali vya uchunguzi wa kifaa cha kunakili data za ndege kwa kiingereza Blackbox.
Kwa mujibu wa taarifa ya mmoja wa wachunguzi kuna mfanano mkubwa baina ya jinsi ajali hiyo ilivyotokea na ile iliyohusisha ndege sawa na hiyo ya 737-8-Max mwaka uliopita nchini Indonesia.