Na Beatrice Maganga, Willy Khaemba
Polisi mjini Eldoret wamemtia mbaroni mwanamume mwenye umri wa miaka 36 anayedaiwa kumuua mpenziwe mwenye umri wa miaka 26 kwenye Mtaa wa Kapsoya. Mshukiwa wa mauaji ametambuliwa kuwa David Siloba. Polisi wanasema mwili wa marehemu ulitumbukizwa katika tangi la maji huku ukiwa na majeraha mabaya kichwani na vidole kukatwa.