Mahakama ya Kibera memwachilia huru Gavana wa Migoro Okoth Obado kwa bondi ya shilingi laki tano na mdhamini wa kiasi sawa na hicho au thamana ya shilingi laki mbili pesa taslimu.
Akitoa uamuzi huo, hakimu Joyce Gandani amefutilia mbali ombi lililowasilishwa na upande wa mashtaka ukitaka Obado aendelee kuzuiliwa kwa siku kumi na tano zaidi ili kuwapa nafasi kukamilisha uchunguzi. Katika uamuzi huo, Obado hata hivyo ameonywa dhidi ya kuwaingilia mashahidi.