Huduma katika Idara ya Polisi zinaendelea kupigwa jeki kufuatia mipango mipya ambayo imezinduziliwa leo hii.
Sasa Wakenya wataweza kupiga ripoti kuhusu ukosefu wa nidhamu miongoni mwa maafisa wa polisi kwa njia ya kielektroniki bila kujitambulisha. Katika mpango huo mpya, Mkenya yeyote anaweza kutuma ujumbe mfupi kwa nambari 40683 au kupiga simu kwa 0800721230, baada ya hapo atapewa kodi maalum ambapo anaweza kufuatilia malalamiko yake.