Maafisa wa polisi wamemtia mbaroni mwajiri wa Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu Cosmas Mutua , kufuatia madai ya mwaka jana kuwa alitekwa nyara na watu watatu. Mutua alidai kuwa watu waliomteka nyara walitaka kujua anakoishi Naibu Jaji.
Mkurugenzi wa Idara ya upelelezi DCI, George Kinoti anasema Mutua hakutekwa nyara jinsi anavyodai kwenye taarifa aliyowasilisha katika kituo cha polisi cha Kilimani Novemba 8 mwaka uliopita.