Mrengo wa NASA wasitisha maandamano yao dhidi ya IEBC


Mrengo wa NASA wasitisha maandamano yao dhidi ya IEBC
by Yeri
Mrengo WA NASA umetangaza kusitisha kwa muda maandamano hayo wiki hii na kusema utaanda mikutano ya hadhara kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari, kinara wa NASA, Raila Odinga amesema Ijumaa wiki hii, ambayo ni Siku ya Sikukuu ya Mashujaa, wataandaa mkutano sambamba wa maadhimisho hayo kwa heshima ya waandamanaji waliouliwa wakati wa kushinikiza mageuzi katika Tume ya Uchaguzi, IEBC.
Aidha Odinga ameitaka serikali kusitisha mauaji ya kiholela ya waandamanaji, hasa kwenye maeneo ambayo mrengo huo una ufuasi mkubwa na kutishia kuwachukulia hatua Kaimu Waziri wa Masuala ya Ndani ya Nchi, Fred Matiang'i na Inspekta Mkuu wa Polisi, Joseph Boinnet kwa mauaji hayo.
Aidha Odinga amesema hawezi kushauriana na Rais Uhuru Kenyatta kuhusu suala la serikali ya mseto.?

 

 

Related Topics